Alfred Koech anaye julikana mitandaoni pia kama "Sergent" ni Mkuregenzi Mtendaji wa shirika la Landson Foundation, ambayo huwasaidia vijana wenye vipaji vya riadha kupitia elimu nchini Kenya.
Bw Koech ambaye ni mkaaji wa Perth, Magharibi Australia, alirejea nchini takriban wiki tatu zilizo pita kutoka Kenya, na alikuwa amekutana na marehemu ambaye walikuwa wame weka mipango tayari yakutembelea shule na kambi ya wanariadha ambayo Sergent amejenga nyumbani kwao.
Katika mazungumzo maalum na SBS Swahili, Sergent aliweka wazi hisia zake kwa kifo cha Bw Kiptum na jinsi atakavyo mkumbuka.
Bonyeza hapo juu kwa mahojiano kamili.